Ruka hadi kwenye maudhui makuu

CHADEMA HAIKUBALIANI NA MATOKEO YA UCHAGUZI MKUU 2015


WAKATI  Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC)
ikimtangaza  mshindi wa urais wa Tanzania
katika Uchaguzi Mkuu wa Jumapili iliyopita,
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)
kimeyakataa matokeo hayo.
Kimesema hakitakubali matokeo ya urais
yatakayotangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi
(NEC) kwa madai kuwa mchakato wa kuhesabu
kura umekiukwa na haukufuata sheria. Aidha,
chama hicho kimetaka NEC kusimamisha
kutangaza matokeo hayo kwa kuwa yako kinyume
cha utaratibu.
Akizungumza na waandishi wa habari Dar es
Salaam jana, mgombea urais wa Chadema,
Edward Lowassa alidai utangazaji wa matokeo
hayo umevurugwa na watendaji wa tume hiyo ili
kukisaidia Chama Cha Mapinduzi (CCM).
“Katika maeneo mengi ambako matokeo
yameshatangazwa mpaka sasa, kilichoripotiwa
kwa matokeo ya uchaguzi wa urais, hakifanani
wala kuendana na matakwa halisi ya wananchi.
Matokeo mengi yamesheheni udanganyifu, ulaghai
na yameandaliwa kwa lengo maalumu la kumbeba
mgombea wa CCM, John Pombe Magufuli,” alidai
Lowassa aliyepewa jukumu na umoja wa vyama
vinne vya upinzani maarufu Ukawa kuwania urais.
Alidai tangu awali uongozi wa umoja huo ulikuwa
ukitoa kasoro zilizojitokeza katika uchaguzi, lakini
Tume imeendelea kutangaza matokeo hayo bila
kuchukua hatua ya kushughulikia kasoro hizo.
Alidai kuwa wanaamini wao walikuwa wana uwezo
wa kushinda kwa zaidi ya asilimia 60. “Kutokana na
makosa hayo makubwa na ya makusudi
yanayofanywa na watendaji wa NEC, mimi Edward
Ngoyai Lowassa, mgombea urais wa Jamhuri ya
Muungano na mgombea mwenza, Juma Duni Haji,
tunautangazia umma wa Watanzania na Jumuiya
ya Kimataifa, kwamba hatukubaliani na matokeo
yanayotangazwa na NEC,” alisema.
Duni ambaye kabla ya kujiunga na Chadema
alikuwa mwanachama na kiongozi wa Chama cha
Wananchi (CUF), alisema hawatakubaliana na
matokeo hayo kwa madai ya kuwa kuna kura hewa
nyingi ambazo zimeongezwa ili kuipa ushindi CCM.
Aidha, alitaka Watanzania na hasa vijana kuwa
watulivu na waendelee kuiheshimu amani iliyopo,
kwa kuwa viongozi hao bado wanajadiliana ili kujua
hatua za kuchukua.
MAHANAIMU BLOG

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

CHANGAMOTO KATIKA LUGHA YA KISWAHILI KWENYE MAMBO YA KOMPYUTA (TEHAMA)

Changamoto zinazoikabili lugha ya Kiswahili katika Teknolojia ya Habari na Mawasiliano Kila jitihada zinazofanywa katika kufikia malengo fulani huwa hakukosi changamoto. Katika jitihada za kufanya Kiswahili kuwa lugha ya kiteknolojia kumetokea changamoto nyingi, moja wapo iliyo kuu kabisa ni kwamba lugha ya Kiswahili haimilikiwi na taifa lolote tajiri kwa hiyo katika harakatika za kuendeleza inakumbana na changamoto nyingi kama vile ukosefu wa fedha na hata utayari wa viongozi wa kisiasa kukiendeleza Kiswahili ni mdogo sana, hata hivyo harakati hizi zinapingwa na mataifa ambayo lugha zao zimeendelea sana kiteknolojia kwa kuhofia kwamba zitafunikwa na matumizi ya Kiswahili. Wapo tayari kutoa misaada ili kuendeleza lugha zao kukididimiza Kiswahili kitu ambacho kinafanya harakati za kukiendeleza Kiswahili kuwa ngumu kwani nchi kinamozungumzwa Kiswahili hazina pesa za kupambana na mataifa makubwa yanayopigia upatu lugha zao. Kutokana na sababu hizo, kasi ya uundaji wa istilahi za kiteknolo...

MAOMBI YA MWENYE DHAMBI

MAOMBI YA MWENYE THAMBI : Ombi la mwenye dhambi ni gani?" Ombi la mwenye dhambi ni Ombi ambalo mtu huomba kwa Mungu wakati anapotambua ya kwamba yeye ni mwenye dhambi au ametenda thambi na anahitaji kusamehewa na Mwokozi. Kusema Ombi hili la mwenye dhambi haikamilishi tayari kila kitu. Ombi la mwenye dhambi hufanya kazi tu sawasawa linapokuwa limesimamia kile mtu anacho fahamu, anacho elewa, na kukubali kuhusu dhambi zake na hitaji la Wokovu. Hatua ya kwanza ya Ombi la mwenye dhambi ni kufahamu ya kwamba sisi sote ni wenye dhambi. Warumi 3:10 , “Kama ilivyoandikwa,ya kwamba,Hakuna mwenye haki hata mmoja.” Bibilia inaonyesha wazi ya kwamba sisi sote tumefanya dhambi. Sisi sote ni wenye dhambi na tunahitaji rehema na msamaha toka kwa Mungu (Tito 3:5-7). Kwa ajili ya dhambi zetu,tunastahili adhabu ya milele (Mathayo 25:46). Ombi hili la mwenye dhambi ni kwa kutafuta neema badala ya hukumu. Ni ombi la kuulizia rehema badala ya hasira kuu.rehema ni kuhesabiwa ...

YESU NI NANI.

Kuna maswali mengi sana unopo mtaja yesu ila naomba ufuatane pamoja nami hatua moja hadi nyingile ili tumjue yesu ni nani k aribia miaka 2.000 iliyopita Yesu aliwauliza wanafunzi wake maswali maswali mawili ambayo mpaka sasa yamo ndani ya Mioyo na fikra za wanaadamu 1." watu hunena kuwa mwana wa adamu kuwa ni nani ?" 2. na ninyi mwanena mm kuwa ni nani ?" matayo .16:13-16 watu wengi,dini nyingi na hata wasomi wengi(ma-filosofa)wamejaribu kutoa majibu kadhaa  katika kujibu swali la kwanza .baadha ya watu wengine walijibu kuwa yu nabii , na kwa wengine yesu alikuwa mwalimu mkuu na bado kwa wengine alikuwa mtu mwema na mwadilifu ambaye mfano wa maisha yake unastahili kuigwa. Lakini jawabu la swali la pili ni muhimu sana.maana katika jawabu la kila mtu binafsi,ndipo pale penye hatima ya milele ( Yohana3 :36 )lakini haina maana na mawazo ya maisha ya wakati huu( Yohana 10:10; wakolosai3 :3-4; wagalatia2 :20) hivyo ba...