WAKATI Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC)
ikimtangaza mshindi wa urais wa Tanzania
katika Uchaguzi Mkuu wa Jumapili iliyopita,
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)
kimeyakataa matokeo hayo.
Kimesema hakitakubali matokeo ya urais
yatakayotangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi
(NEC) kwa madai kuwa mchakato wa kuhesabu
kura umekiukwa na haukufuata sheria. Aidha,
chama hicho kimetaka NEC kusimamisha
kutangaza matokeo hayo kwa kuwa yako kinyume
cha utaratibu.
Akizungumza na waandishi wa habari Dar es
Salaam jana, mgombea urais wa Chadema,
Edward Lowassa alidai utangazaji wa matokeo
hayo umevurugwa na watendaji wa tume hiyo ili
kukisaidia Chama Cha Mapinduzi (CCM).
“Katika maeneo mengi ambako matokeo
yameshatangazwa mpaka sasa, kilichoripotiwa
kwa matokeo ya uchaguzi wa urais, hakifanani
wala kuendana na matakwa halisi ya wananchi.
Matokeo mengi yamesheheni udanganyifu, ulaghai
na yameandaliwa kwa lengo maalumu la kumbeba
mgombea wa CCM, John Pombe Magufuli,” alidai
Lowassa aliyepewa jukumu na umoja wa vyama
vinne vya upinzani maarufu Ukawa kuwania urais.
Alidai tangu awali uongozi wa umoja huo ulikuwa
ukitoa kasoro zilizojitokeza katika uchaguzi, lakini
Tume imeendelea kutangaza matokeo hayo bila
kuchukua hatua ya kushughulikia kasoro hizo.
Alidai kuwa wanaamini wao walikuwa wana uwezo
wa kushinda kwa zaidi ya asilimia 60. “Kutokana na
makosa hayo makubwa na ya makusudi
yanayofanywa na watendaji wa NEC, mimi Edward
Ngoyai Lowassa, mgombea urais wa Jamhuri ya
Muungano na mgombea mwenza, Juma Duni Haji,
tunautangazia umma wa Watanzania na Jumuiya
ya Kimataifa, kwamba hatukubaliani na matokeo
yanayotangazwa na NEC,” alisema.
Duni ambaye kabla ya kujiunga na Chadema
alikuwa mwanachama na kiongozi wa Chama cha
Wananchi (CUF), alisema hawatakubaliana na
matokeo hayo kwa madai ya kuwa kuna kura hewa
nyingi ambazo zimeongezwa ili kuipa ushindi CCM.
Aidha, alitaka Watanzania na hasa vijana kuwa
watulivu na waendelee kuiheshimu amani iliyopo,
kwa kuwa viongozi hao bado wanajadiliana ili kujua
hatua za kuchukua.
MAHANAIMU BLOG
Changamoto zinazoikabili lugha ya Kiswahili katika Teknolojia ya Habari na Mawasiliano Kila jitihada zinazofanywa katika kufikia malengo fulani huwa hakukosi changamoto. Katika jitihada za kufanya Kiswahili kuwa lugha ya kiteknolojia kumetokea changamoto nyingi, moja wapo iliyo kuu kabisa ni kwamba lugha ya Kiswahili haimilikiwi na taifa lolote tajiri kwa hiyo katika harakatika za kuendeleza inakumbana na changamoto nyingi kama vile ukosefu wa fedha na hata utayari wa viongozi wa kisiasa kukiendeleza Kiswahili ni mdogo sana, hata hivyo harakati hizi zinapingwa na mataifa ambayo lugha zao zimeendelea sana kiteknolojia kwa kuhofia kwamba zitafunikwa na matumizi ya Kiswahili. Wapo tayari kutoa misaada ili kuendeleza lugha zao kukididimiza Kiswahili kitu ambacho kinafanya harakati za kukiendeleza Kiswahili kuwa ngumu kwani nchi kinamozungumzwa Kiswahili hazina pesa za kupambana na mataifa makubwa yanayopigia upatu lugha zao. Kutokana na sababu hizo, kasi ya uundaji wa istilahi za kiteknolo...
Maoni
Chapisha Maoni