Wednesday, November 4, 2015
Tupe Maoni Yako( Matusi
Hapana )
Mpekuzi blog
Serikali Yakanusha Taarifa za Kifo
cha Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa
Msemaji Mkuu wa Serikali ya Tanzania, Assah
Mwambene amekanusha taarifa zinazosambaa
katika mitandao ya kijamii kuhusu Rais Mstaafu,
Benjamin Mkapa kuwa amefariki Dunia.
Akizungunza na waandishi wa habari katika ukumbi
wa Habari Maelezo jijini Dar es Salaam, Mwambene
amesema Rais Mkapa yupo salama na mzima wa
afya na hakuna maradhi yoyote yanayomsumbua.
Mwambene amewaasa watumiaji wa mitandao
mbalimbali hasa Blogs kuacha kuitumia mitandao
hiyo kwa kupotosha umma na kuandika nambo
yasiyo na ukweli ili kuepusha mifumuko ya habari
za upotishaji.
“Si jambo jema na wanaofanya hivyo waache mara
moja kabla ya hatua stahiki hazijachukuliwa,”
amesema Mwambene.
Amesema kuwa jambo la kumzushia mtu kifo si
jambo zuri ambalo amelizungumza kama ‘uchuro’
kwa mtu husika na kumtabiria mabaya.
“Mkapa yupo hai na kesho pia atakuwepo katika
sherehe za kumuapisha Rais mteule wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, John Magufuli,” amesema
Mwmbene na kuongeza.
Serikali italishughulikia hili na tayari imeshaanza
kukamata baadhi ya watu mbalimbali ambao
wanatoa taarifa za uongo zinazopelekea umma
kupotoka.
Amesema kuwa vyombo vya habari vifanye kazi
kwa uweredi ili kazi ya uandishi wao iwe ya usawa
na kufuata misingi ya uandishi, jambo ambalo
wengi hukiuka kutokana kutofuata weredi wa kazi
zao.
Changamoto zinazoikabili lugha ya Kiswahili katika Teknolojia ya Habari na Mawasiliano Kila jitihada zinazofanywa katika kufikia malengo fulani huwa hakukosi changamoto. Katika jitihada za kufanya Kiswahili kuwa lugha ya kiteknolojia kumetokea changamoto nyingi, moja wapo iliyo kuu kabisa ni kwamba lugha ya Kiswahili haimilikiwi na taifa lolote tajiri kwa hiyo katika harakatika za kuendeleza inakumbana na changamoto nyingi kama vile ukosefu wa fedha na hata utayari wa viongozi wa kisiasa kukiendeleza Kiswahili ni mdogo sana, hata hivyo harakati hizi zinapingwa na mataifa ambayo lugha zao zimeendelea sana kiteknolojia kwa kuhofia kwamba zitafunikwa na matumizi ya Kiswahili. Wapo tayari kutoa misaada ili kuendeleza lugha zao kukididimiza Kiswahili kitu ambacho kinafanya harakati za kukiendeleza Kiswahili kuwa ngumu kwani nchi kinamozungumzwa Kiswahili hazina pesa za kupambana na mataifa makubwa yanayopigia upatu lugha zao. Kutokana na sababu hizo, kasi ya uundaji wa istilahi za kiteknolo...
Maoni
Chapisha Maoni