Ruka hadi kwenye maudhui makuu

November 14, 2015 Mambo yameanza Dodoma, ratiba ya Bunge ni hii + pichaz Wabunge waliofika.. Newsroom TZA Kama umetembelea mitandao ya kijamii utakuwa umeona pilikapilika za kinachoendelea Dodoma sasahivi, baada ya Uchaguzi Mkuu kuisha wale wote waliopita kwenye nafasi ya Ubunge wanasubiri shughuli ya kuapishwa halafu Vikao vya Bunge vinaanza. Nimeipata Ratiba ya kitakachoendelea Dodoma kwa jumla ya siku saba mfululizo, yani kuanzia jana November 13 mpaka November 20 2015… Ratiba yenyewe hii hapa. Mbunge Mteule wa Jimbo Mwanga K’njaro, Prof. Jumanne Maghembe akiwasilisha nyaraka zake wakati wa kusajiliwa Bungeni Dodoma. Mbunge Mteule wa Sengerema, William Ngeleja nae kwenye foleni ya usajili katika Viwanja vya Bunge Dodoma

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAOMBI YA MWENYE DHAMBI

MAOMBI YA MWENYE THAMBI : Ombi la mwenye dhambi ni gani?" Ombi la mwenye dhambi ni Ombi ambalo mtu huomba kwa Mungu wakati anapotambua ya kwamba yeye ni mwenye dhambi au ametenda thambi na anahitaji kusamehewa na Mwokozi. Kusema Ombi hili la mwenye dhambi haikamilishi tayari kila kitu. Ombi la mwenye dhambi hufanya kazi tu sawasawa linapokuwa limesimamia kile mtu anacho fahamu, anacho elewa, na kukubali kuhusu dhambi zake na hitaji la Wokovu. Hatua ya kwanza ya Ombi la mwenye dhambi ni kufahamu ya kwamba sisi sote ni wenye dhambi. Warumi 3:10 , “Kama ilivyoandikwa,ya kwamba,Hakuna mwenye haki hata mmoja.” Bibilia inaonyesha wazi ya kwamba sisi sote tumefanya dhambi. Sisi sote ni wenye dhambi na tunahitaji rehema na msamaha toka kwa Mungu (Tito 3:5-7). Kwa ajili ya dhambi zetu,tunastahili adhabu ya milele (Mathayo 25:46). Ombi hili la mwenye dhambi ni kwa kutafuta neema badala ya hukumu. Ni ombi la kuulizia rehema badala ya hasira kuu.rehema ni kuhesabiwa ...

CHANGAMOTO KATIKA LUGHA YA KISWAHILI KWENYE MAMBO YA KOMPYUTA (TEHAMA)

Changamoto zinazoikabili lugha ya Kiswahili katika Teknolojia ya Habari na Mawasiliano Kila jitihada zinazofanywa katika kufikia malengo fulani huwa hakukosi changamoto. Katika jitihada za kufanya Kiswahili kuwa lugha ya kiteknolojia kumetokea changamoto nyingi, moja wapo iliyo kuu kabisa ni kwamba lugha ya Kiswahili haimilikiwi na taifa lolote tajiri kwa hiyo katika harakatika za kuendeleza inakumbana na changamoto nyingi kama vile ukosefu wa fedha na hata utayari wa viongozi wa kisiasa kukiendeleza Kiswahili ni mdogo sana, hata hivyo harakati hizi zinapingwa na mataifa ambayo lugha zao zimeendelea sana kiteknolojia kwa kuhofia kwamba zitafunikwa na matumizi ya Kiswahili. Wapo tayari kutoa misaada ili kuendeleza lugha zao kukididimiza Kiswahili kitu ambacho kinafanya harakati za kukiendeleza Kiswahili kuwa ngumu kwani nchi kinamozungumzwa Kiswahili hazina pesa za kupambana na mataifa makubwa yanayopigia upatu lugha zao. Kutokana na sababu hizo, kasi ya uundaji wa istilahi za kiteknolo...

Serikali ya kishetani

Shetani yuko duniani, na anafanya kazi duniani. Watu wengi wanapokua wanapambana na shetani wanakua wanawaza kwamba yuko mbali sana na wao. Shetani amewakilishwa na majina mbali mbali katika biblia; mfano > Shetani > Ibilisi > Mwovu Shahidi nane kibiblia zinazoonyesha shetani anakaa duniani. 1. Shetani alitupwa duniani Ufunuo 12:12 2. Shimo la kuzimu lipo hapa hapa duniani Ufunuo 9:1-2,11 3. Siku moja alionekana duniani anazunguka zunguka. Ayubu 1:7, ayubu 2:2 Shetani anazunguka zunguka na pia anatembea tembea. Hivyo unaweza kukutana nae anatembea, au anazunguka zunguka. Bwana aliongea na shetani ili sisi tuweze kujifunza kutoka Kwenye maongezi yake. 4. Shetani aligombania mwili kwenye mazishi. Kumbu 34:1-6 Hapa biblia inaonyesha Musa amekufa,na Mungu akamzika. Lakini Yuda 1:9 shetani akashindana na mikaeli kwa ajili ya mwili wa Musa. 5. Shetani aliingia kwenye ibada wakati Kuhani mkuu Yoshua akiendesha ibada Zekaria 3:1-2 6. Shetani aliongea na Daudi. 1 Nyakati 21:1 7. Duni...