Ndugu Mpendwa kwa pamoja Tunakukaribisha sana katika
Safu hii Fahamu yakwamba Tupo hapa kwaajili yako na kwa
msaada zaidi wa Ushahuri au Maombezi ya mahitaji mbali
mbali Masaa 24 siku 7 za wiki, Piga No:
0756809209/0786608801/0653294219 Itapokelewa na
Mtumishi wa Mungu mwenyewe Samson mboya,
Calivary
Assemblies of
God - Geita
Nyankumbu-
(Hema ya
kinabii )
Newer Post Older Post Home
NENO LA MUNGU LINA NENA NINI JUU YA
USHOGA?
Je, Neno la Mungu lina nena nini juu ya ushoga ? Je, ni(
dhambi?)
Biblia inasisitiza kila mara kwamba ushoga ni dhambi
(mwanzo 19:1-13; mambo ya walawi 18: 22; warumi
1:26-27; wakorintho wa kwanza 6:9). Warumi 1:26-27
inatufundisha ya kwamba ushoga ni njia mojawapo ya
kumkana na kutomtii Mungu. Mtu anapodumu katika dhambi
na kutokuamini biblia inatuambia ya kwamba “Mungu
huwaachilia” kutenda maovu zaidi ili wapate kujua ubatili wa
maisha bila Uwepo wa Mungu. Wakorintho wa kwanza 6:9
inasema kuwa mashoga hawataurithi ufalme wa Mungu.
Mungu haumbi mwanadamu mwenye tamaa ya ushoga.
Biblia inatuambia mtu huwa shoga kwa sababu ya dhambi.
(warumi 1:24-27), na pia kwa sababu ya uamuzi wake
mwenyewe. Mtu anaweza kuzaliwa na msukumo juu ya
ushoga
kama vile watu pia huzaliwa na msukumo juu ya
fujo na dhambi nyinginezo. Hili halihalalishi dhambi yoyote
inayofanywa na wanadamu. Je, mtu akizaliwa na msukumo
wa hasira mbaya, ni halali aendeleze hasira zake mbaya? La,
hasha. Hata kwa ushoga pia si halali.
Hata hivyo Biblia haiitaji dhambi ya ushoga kuwa ndiyo
kubwa zaidi. Kila dhambi ni chukizo kwa Mungu. Ushoga ni
mojawapo ya mambo yaliyoorodheshwa katika wakorintho
wa kwanza 6:9-10 yatakayozuia mtu asiingie katika ufalme
wa Mungu. Kulingana na Biblia msamaha wa Mungu juu ya
shoga upo sawa na wa mzinzi, muabudu sanamu, muuaji,
mwizi na kadhalika. Mungu tena aahidi uwezo juu ya
kushinda dhambi, pamoja na ushoga , kwa wale wote
watakao mwaminiYesu kristo kwa wokovu wao (wakorintho
wa kwanza 6:11; wakorintho wa pili 5:17).
Sina maana ya kufuatilia maisha ya mtu lah! Bali ni mimi
ninatumika tu kufikisha ujumbe kwa jamii yetu na nina amini
hata mashoga matatembelea hii Safu bila shaka itanamsaidia
mwenye tabia hii ya ushoga kuiacha mara moja
,japo wapo wengine ambao sijazungumzia sana
hapa ila watakuwa wameelezewa ukurasa mwingine wale
wanao lawiti, watoto,wadogo,wake zao au wake za watu
wengine kwa yeyote anayefanya tendo hili ni vema kama
ulikuwa haufahamu fahamu sasa kuwa unafanya chukizo
mbele ya uso wa Mungu, acha mara moja na utubu kabisa,
Changamoto zinazoikabili lugha ya Kiswahili katika Teknolojia ya Habari na Mawasiliano Kila jitihada zinazofanywa katika kufikia malengo fulani huwa hakukosi changamoto. Katika jitihada za kufanya Kiswahili kuwa lugha ya kiteknolojia kumetokea changamoto nyingi, moja wapo iliyo kuu kabisa ni kwamba lugha ya Kiswahili haimilikiwi na taifa lolote tajiri kwa hiyo katika harakatika za kuendeleza inakumbana na changamoto nyingi kama vile ukosefu wa fedha na hata utayari wa viongozi wa kisiasa kukiendeleza Kiswahili ni mdogo sana, hata hivyo harakati hizi zinapingwa na mataifa ambayo lugha zao zimeendelea sana kiteknolojia kwa kuhofia kwamba zitafunikwa na matumizi ya Kiswahili. Wapo tayari kutoa misaada ili kuendeleza lugha zao kukididimiza Kiswahili kitu ambacho kinafanya harakati za kukiendeleza Kiswahili kuwa ngumu kwani nchi kinamozungumzwa Kiswahili hazina pesa za kupambana na mataifa makubwa yanayopigia upatu lugha zao. Kutokana na sababu hizo, kasi ya uundaji wa istilahi za kiteknolo...
Maoni
Chapisha Maoni