Serikali imesema madaktari wote watakaopata nafasi ya kusoma nje ya nchi kwa ufadhili wake, watafanya hivyo kwa kusaini mkataba.
Kufanya hivyo kumeelezewa kuwa kutasaidia kuwabana wale wanaohitimu na kutimkia nje ya nchi kwenda kufanya kazi huko.
Hayo yalisemwa na Naibu Waziri wa Afya, Jinsia, Maendeleo ya Jamii, Wazee na Watoto, Dk Hamis Kigwangalah alipotembelea Manispaa ya Shinyanga.
Alisema Serikali imeendelea kuwapoteza madaktari wengi inaowasomesha wanaokimbia kwa madai ya mazingira mabovu ya kufanyia kazi.
Wengi wao hukimbilia nchi za Afrika Kusini na Botswana wanakodai kuna mazingira mazuri ya kufanyia kazi.
Alisema wanataka kuona wizara inakuwa na madaktari bingwa wa kutosha kulika ilivyo sasa.
Awali, Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Mkoa wa Shinyanga, Fredrick Mlekwa alimwambia naibu waziri huyo kuwa, tatizo kubwa linalokwamisha utendaji kazi wao ni upungufu wa madaktari hospitali hapo.
Dk Mlekwa alisema hospitali hiyo ina madaktari bingwa wanne, madaktari wa kawaida 15 na madaktari wasaidizi kumi na moja. Alisema kwa mwaka hutoa huduma kwa wagonjwa zaidi ya 500,000.
Changamoto zinazoikabili lugha ya Kiswahili katika Teknolojia ya Habari na Mawasiliano Kila jitihada zinazofanywa katika kufikia malengo fulani huwa hakukosi changamoto. Katika jitihada za kufanya Kiswahili kuwa lugha ya kiteknolojia kumetokea changamoto nyingi, moja wapo iliyo kuu kabisa ni kwamba lugha ya Kiswahili haimilikiwi na taifa lolote tajiri kwa hiyo katika harakatika za kuendeleza inakumbana na changamoto nyingi kama vile ukosefu wa fedha na hata utayari wa viongozi wa kisiasa kukiendeleza Kiswahili ni mdogo sana, hata hivyo harakati hizi zinapingwa na mataifa ambayo lugha zao zimeendelea sana kiteknolojia kwa kuhofia kwamba zitafunikwa na matumizi ya Kiswahili. Wapo tayari kutoa misaada ili kuendeleza lugha zao kukididimiza Kiswahili kitu ambacho kinafanya harakati za kukiendeleza Kiswahili kuwa ngumu kwani nchi kinamozungumzwa Kiswahili hazina pesa za kupambana na mataifa makubwa yanayopigia upatu lugha zao. Kutokana na sababu hizo, kasi ya uundaji wa istilahi za kiteknolo...
Maoni
Chapisha Maoni