SAKATA la wafanyabiashara watano waliogoma kulipa kodi ndani ya muda uliowekwa na Rais John Magufuli limechukua sura mpya baada ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kuwakabidhi kwenye vyombo vya dola kwa hatua za kisheria.
Wafanyabiashara hao ni miongoni mwa 43 ambao awali walitajwa kupitisha makontena 329 bandarini bila kuyalipia kodi.
Mwishoni mwa mwaka jana, Rais Magufuli alitoa siku saba wajisalimishe wenyewe kulipa kodi kwa TRA bila adhabu.
Akizungumza na Nipashe ofisini kwake jana jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi TRA, Richard Kayombo alisema kutokana na muda uliotolewa kuisha na wafanyabiashara hao kushindwa kutekeleza walichoagizwa vyombo vya dola vinaendelea kulifanyia kazi suala hilo ili hatua za kisheria zichukuliwe.
Alisema wameamua kuvishirikisha vyombo vya dola kwa sababu wafanyabiashara hao wamekiuka agizo lililotolewa awali la kuwataka walipe kodi kwa hiyari yao ndani ya muda waliopewa.
Alisema makampuni ya wafanyabiashara hao, matatu yalichukua makadirio ya kodi wanayodaiwa na serikali lakini hayakwenda kulipa na mawili hayakuchukua kabisa.
Alisisitiza kuwa mpaka sasa fedha ambazo zimeshalipwa ni zaidi ya Sh. bilioni 11.9 ambapo wapo waliolipa zote na wengine kulipa sehemu ya malipo.
“Wafanyabiashara 19 wamelipa fedha zote walizokuwa wanadaiwa na wengine 19 wamelipa sehemu ya malipo, lakini wengine wamegoma wanahoji kulipa sehemu za adhabu,” alisema. “Mazungumzo yanaendelea kuhusu wafanyabiashara hao.”
Mwishoni mwa mwaka jana, Rais Magufuli alitoa siku saba kwa wafanyabiashara hao kulipa kodi na kwamba mara baada ya muda huo kupita hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yao.
Makontena hayo yaliondolewa bila kulipiwa kodi katika Bandari Kavu kadhaa, ikiwemo ya Azam inayomilikuwa na mfanyabiashara Said Salim Bakhresa.
Changamoto zinazoikabili lugha ya Kiswahili katika Teknolojia ya Habari na Mawasiliano Kila jitihada zinazofanywa katika kufikia malengo fulani huwa hakukosi changamoto. Katika jitihada za kufanya Kiswahili kuwa lugha ya kiteknolojia kumetokea changamoto nyingi, moja wapo iliyo kuu kabisa ni kwamba lugha ya Kiswahili haimilikiwi na taifa lolote tajiri kwa hiyo katika harakatika za kuendeleza inakumbana na changamoto nyingi kama vile ukosefu wa fedha na hata utayari wa viongozi wa kisiasa kukiendeleza Kiswahili ni mdogo sana, hata hivyo harakati hizi zinapingwa na mataifa ambayo lugha zao zimeendelea sana kiteknolojia kwa kuhofia kwamba zitafunikwa na matumizi ya Kiswahili. Wapo tayari kutoa misaada ili kuendeleza lugha zao kukididimiza Kiswahili kitu ambacho kinafanya harakati za kukiendeleza Kiswahili kuwa ngumu kwani nchi kinamozungumzwa Kiswahili hazina pesa za kupambana na mataifa makubwa yanayopigia upatu lugha zao. Kutokana na sababu hizo, kasi ya uundaji wa istilahi za kiteknolo...
Maoni
Chapisha Maoni