Ruka hadi kwenye maudhui makuu

MAGUFULI ATAKIWA KUZUIA UNYWAJI WA POMBE WAKAZI WA KAZI

WAKAZI wa Jiji la Arusha wamemtaka Rais
Mteule, Dk John Magufuli kuhakikisha anasimamia
utekelezaji na uwajibikaji kwa kila Mtanzania na
kupiga vita baa na vijiwe vya kahawa kufunguliwa
wakati wa kazi.
Mmoja wa wakazi wa Jiji la Arusha anayeishi
Moshono, Julius Mollel alisema kuwa katika miaka
ya 1970 hadi 1980 sehemu zote za starehe
zikiwemo baa na vijiwe vya kahawa vilikuwa
vikifunguliwa baada ya kazi.
Mollel alisema nyakati hizo wakuu wa mikoa,
wakuu wa wilaya na wakurugenzi wa jiji na
halmashauri walikuwa mstari wa mbele kusimamia
sheria hiyo na kila mtu alikuwa akiwajibika kwa
kufanya kazi bila kusukumwa.
Alisema kwa sasa inashangaza kuona Jiji la
Arusha toka asubuhi baa na maduka ya pombe
yako wazi. Katika vijiwe vya kahawa watu wamejaa
wanazungumza siasa na kushindwa kufanya kazi
na kubaki kulalamika hovyo hovyo.
‘’Ninamwomba Magufuli awaagize watendaji wa
serikali ngazi ya Jiji, Wilaya na Mkoa kusimamia
sheria za muda wa kazi kufanya kazi na kuacha
kunywa pombe,‘’ alisema.
Naye Peter Massawe alisema kuwa uzembe uliopo
kwa watendaji wa serikali katika jiji na halmashauri
kwa kushindwa kusimamia sheria hiyo ndio
umefanya Arusha watu kuanza kunywa pombe
kuanzia asubuhi.
Massawe ambaye ni mkazi wa Sanawari alisema
kuwa wakazi wa Arusha wameshazoea kunywa
pombe kuanzia asubuhi na sasa wanaona kama ni
haki yao kufanya hivyo wakati hilo ni kosa.
Alisema kuwa enzi za Baba wa Taifa, Mwalimu
Julius Nyerere, sehemu zote za starehe zilikuwa
zikiruhusiwa kufunguliwa baada ya saa 8:00
mchana na muda wote watu wanatakiwa kufanya
kazi na sio kukaa baa.
Juma Masoud mkazi wa kata ya Kati alisema
inasikitisha kuona wakazi wa Arusha kucha kutwa
wanakunywa pombe na kunywa kahawa kuanzia
asubuhi.
Masoud alisema wala rushwa wamejaa katika
halmashauri na jiji na kushindwa kusimamia hilo
hivyo Magufuli anapaswa kuwawajibisha
wanaoshindwa kusimamia sheria ya kufanya kazi
na kuacha watu wakinywa pombe asubuhi.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

CHANGAMOTO KATIKA LUGHA YA KISWAHILI KWENYE MAMBO YA KOMPYUTA (TEHAMA)

Changamoto zinazoikabili lugha ya Kiswahili katika Teknolojia ya Habari na Mawasiliano Kila jitihada zinazofanywa katika kufikia malengo fulani huwa hakukosi changamoto. Katika jitihada za kufanya Kiswahili kuwa lugha ya kiteknolojia kumetokea changamoto nyingi, moja wapo iliyo kuu kabisa ni kwamba lugha ya Kiswahili haimilikiwi na taifa lolote tajiri kwa hiyo katika harakatika za kuendeleza inakumbana na changamoto nyingi kama vile ukosefu wa fedha na hata utayari wa viongozi wa kisiasa kukiendeleza Kiswahili ni mdogo sana, hata hivyo harakati hizi zinapingwa na mataifa ambayo lugha zao zimeendelea sana kiteknolojia kwa kuhofia kwamba zitafunikwa na matumizi ya Kiswahili. Wapo tayari kutoa misaada ili kuendeleza lugha zao kukididimiza Kiswahili kitu ambacho kinafanya harakati za kukiendeleza Kiswahili kuwa ngumu kwani nchi kinamozungumzwa Kiswahili hazina pesa za kupambana na mataifa makubwa yanayopigia upatu lugha zao. Kutokana na sababu hizo, kasi ya uundaji wa istilahi za kiteknolo...

MAOMBI YA MWENYE DHAMBI

MAOMBI YA MWENYE THAMBI : Ombi la mwenye dhambi ni gani?" Ombi la mwenye dhambi ni Ombi ambalo mtu huomba kwa Mungu wakati anapotambua ya kwamba yeye ni mwenye dhambi au ametenda thambi na anahitaji kusamehewa na Mwokozi. Kusema Ombi hili la mwenye dhambi haikamilishi tayari kila kitu. Ombi la mwenye dhambi hufanya kazi tu sawasawa linapokuwa limesimamia kile mtu anacho fahamu, anacho elewa, na kukubali kuhusu dhambi zake na hitaji la Wokovu. Hatua ya kwanza ya Ombi la mwenye dhambi ni kufahamu ya kwamba sisi sote ni wenye dhambi. Warumi 3:10 , “Kama ilivyoandikwa,ya kwamba,Hakuna mwenye haki hata mmoja.” Bibilia inaonyesha wazi ya kwamba sisi sote tumefanya dhambi. Sisi sote ni wenye dhambi na tunahitaji rehema na msamaha toka kwa Mungu (Tito 3:5-7). Kwa ajili ya dhambi zetu,tunastahili adhabu ya milele (Mathayo 25:46). Ombi hili la mwenye dhambi ni kwa kutafuta neema badala ya hukumu. Ni ombi la kuulizia rehema badala ya hasira kuu.rehema ni kuhesabiwa ...

YESU NI NANI.

Kuna maswali mengi sana unopo mtaja yesu ila naomba ufuatane pamoja nami hatua moja hadi nyingile ili tumjue yesu ni nani k aribia miaka 2.000 iliyopita Yesu aliwauliza wanafunzi wake maswali maswali mawili ambayo mpaka sasa yamo ndani ya Mioyo na fikra za wanaadamu 1." watu hunena kuwa mwana wa adamu kuwa ni nani ?" 2. na ninyi mwanena mm kuwa ni nani ?" matayo .16:13-16 watu wengi,dini nyingi na hata wasomi wengi(ma-filosofa)wamejaribu kutoa majibu kadhaa  katika kujibu swali la kwanza .baadha ya watu wengine walijibu kuwa yu nabii , na kwa wengine yesu alikuwa mwalimu mkuu na bado kwa wengine alikuwa mtu mwema na mwadilifu ambaye mfano wa maisha yake unastahili kuigwa. Lakini jawabu la swali la pili ni muhimu sana.maana katika jawabu la kila mtu binafsi,ndipo pale penye hatima ya milele ( Yohana3 :36 )lakini haina maana na mawazo ya maisha ya wakati huu( Yohana 10:10; wakolosai3 :3-4; wagalatia2 :20) hivyo ba...