Ruka hadi kwenye maudhui makuu

LUKUVI AOMBWA KUFUTA HATI YA SHAMBA

Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi ameombwa kufuta hati ya shamba la mwekezaji katika Kijiji cha Kenyana Kata ya Ring’wani wilayani hapa Mkoa wa Mara kwa madai ya kushindwa kuliendeleza. Wakizungumza kwenye mkutano wa hadhara na diwani wa kata hiyo, Maiso Mahemba, wakazi wa kijiji hicho walidai eneo hilo ambalo limechukuliwa na mwekezaji huyo miaka 29 iliyopita, linatakiwa kubatilishwa matumizi kutoka uwekezaji ili liwe na umma. Walisema ni vema Serikali ikawaruhusu wajenge shule ya msingi kwa ajili ya watoto wao ambao hawajaanza masomo. Mmoja wa wakazi hao, Enock Magoiga alisema: “Mwekezaji huyo ana faida gani kwa wananchi kama amechukua eneo halafu hajawahi kuonekana wala kuliendeleza. Tunazuiwa kufanya maendeleo bila sababu za msingi, tunaomba Waziri William Lukuvi afute hati hiyo.” Alisema mazingira hayo yamechangia shule waliyojenga kukataliwa kufunguliwa kwa madai kuwa wamejenga kwenye eneo la mwekezaji na kwamba matokeo yake watoto wao zaidi ya 800 wengi wakiwa na umri zaidi ya miaka 12, hawajaanza masomo. Diwani Mahemba alisema tangu mwaka 1992 wakazi hao waliingia katika eneo hilo kwa kupokelewa na Serikali na kuanza kujenga makazi yao. Alisema baadaye walitambuliwa na kupewa kitongoji hicho, kwa kutumia nguvu zao waliamua kujenga shule hiyo, lakini imezuiwa kufunguliwa kwa misingi ya ubaguzi wa kikabila. Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji cha Kenyana, Matiko Nsaho alithibitisha kuwa eneo hilo lina hati ya muda mrefu na linamilikiwa na raia wa Finland ambaye kwa sasa ni marehemu. Kaimu Ofisa Elimu Wilaya hiyo, Wanyancha Nyakoge alisema waraka namba 5 wa Mwaka 2015 kupitia mwongozo wa utekelezaji unaagiza maeneo ambayo yako mbali na shule wanatakiwa kuanzisha shule shinikizi kuanzia darasa la awali hadi darasa la pili.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAOMBI YA MWENYE DHAMBI

MAOMBI YA MWENYE THAMBI : Ombi la mwenye dhambi ni gani?" Ombi la mwenye dhambi ni Ombi ambalo mtu huomba kwa Mungu wakati anapotambua ya kwamba yeye ni mwenye dhambi au ametenda thambi na anahitaji kusamehewa na Mwokozi. Kusema Ombi hili la mwenye dhambi haikamilishi tayari kila kitu. Ombi la mwenye dhambi hufanya kazi tu sawasawa linapokuwa limesimamia kile mtu anacho fahamu, anacho elewa, na kukubali kuhusu dhambi zake na hitaji la Wokovu. Hatua ya kwanza ya Ombi la mwenye dhambi ni kufahamu ya kwamba sisi sote ni wenye dhambi. Warumi 3:10 , “Kama ilivyoandikwa,ya kwamba,Hakuna mwenye haki hata mmoja.” Bibilia inaonyesha wazi ya kwamba sisi sote tumefanya dhambi. Sisi sote ni wenye dhambi na tunahitaji rehema na msamaha toka kwa Mungu (Tito 3:5-7). Kwa ajili ya dhambi zetu,tunastahili adhabu ya milele (Mathayo 25:46). Ombi hili la mwenye dhambi ni kwa kutafuta neema badala ya hukumu. Ni ombi la kuulizia rehema badala ya hasira kuu.rehema ni kuhesabiwa ...

CHANGAMOTO KATIKA LUGHA YA KISWAHILI KWENYE MAMBO YA KOMPYUTA (TEHAMA)

Changamoto zinazoikabili lugha ya Kiswahili katika Teknolojia ya Habari na Mawasiliano Kila jitihada zinazofanywa katika kufikia malengo fulani huwa hakukosi changamoto. Katika jitihada za kufanya Kiswahili kuwa lugha ya kiteknolojia kumetokea changamoto nyingi, moja wapo iliyo kuu kabisa ni kwamba lugha ya Kiswahili haimilikiwi na taifa lolote tajiri kwa hiyo katika harakatika za kuendeleza inakumbana na changamoto nyingi kama vile ukosefu wa fedha na hata utayari wa viongozi wa kisiasa kukiendeleza Kiswahili ni mdogo sana, hata hivyo harakati hizi zinapingwa na mataifa ambayo lugha zao zimeendelea sana kiteknolojia kwa kuhofia kwamba zitafunikwa na matumizi ya Kiswahili. Wapo tayari kutoa misaada ili kuendeleza lugha zao kukididimiza Kiswahili kitu ambacho kinafanya harakati za kukiendeleza Kiswahili kuwa ngumu kwani nchi kinamozungumzwa Kiswahili hazina pesa za kupambana na mataifa makubwa yanayopigia upatu lugha zao. Kutokana na sababu hizo, kasi ya uundaji wa istilahi za kiteknolo...

Serikali ya kishetani

Shetani yuko duniani, na anafanya kazi duniani. Watu wengi wanapokua wanapambana na shetani wanakua wanawaza kwamba yuko mbali sana na wao. Shetani amewakilishwa na majina mbali mbali katika biblia; mfano > Shetani > Ibilisi > Mwovu Shahidi nane kibiblia zinazoonyesha shetani anakaa duniani. 1. Shetani alitupwa duniani Ufunuo 12:12 2. Shimo la kuzimu lipo hapa hapa duniani Ufunuo 9:1-2,11 3. Siku moja alionekana duniani anazunguka zunguka. Ayubu 1:7, ayubu 2:2 Shetani anazunguka zunguka na pia anatembea tembea. Hivyo unaweza kukutana nae anatembea, au anazunguka zunguka. Bwana aliongea na shetani ili sisi tuweze kujifunza kutoka Kwenye maongezi yake. 4. Shetani aligombania mwili kwenye mazishi. Kumbu 34:1-6 Hapa biblia inaonyesha Musa amekufa,na Mungu akamzika. Lakini Yuda 1:9 shetani akashindana na mikaeli kwa ajili ya mwili wa Musa. 5. Shetani aliingia kwenye ibada wakati Kuhani mkuu Yoshua akiendesha ibada Zekaria 3:1-2 6. Shetani aliongea na Daudi. 1 Nyakati 21:1 7. Duni...