Ruka hadi kwenye maudhui makuu

WAFUASI WAMTAKA MAALIM AITISHE MKUTANO KUMTAMBUA LIPUMBA

Wafuasi wataka Maalim aitishe mkutano kumtambua Lipumba

Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad 

Baadhi ya wafuasi wa aliyekuwa mwenyekiti wa CUF wamesema ili Katibu Mkuu wa chama hicho, Maalim Seif Sharif Hamad aweze kuingia katika ofisi za makao ya CUF Buguruni ni lazima aitishe mkutano na wanahabari kumtambua Profesa Lipumba.

Baadhi ya wafuasi hapo wamekusanyika eneo la ofisi hiyo wakiwa na nia ya kumpokea Profesa Lipumba na kumzuia Maalim Seif endapo atafika.

Akizungumza kwa niaba ya wenzake Juma Yassin amesema Maalim Seif ataendelea kubaki Zanzibar iwapo  hatataka kumtambua Profesa Lipumba ambaye ni mwenyekiti halali Kikatiba.
"Tumesikia leo huenda akaja lakini ofisi  na asijisumbue tupo tayari kwa lolote hadi amtambue Profesa Lipumba," amesema Yassin ambaye ni mwenyekiti wa Tawi la Kosovo Manzese.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

MAOMBI YA MWENYE DHAMBI

MAOMBI YA MWENYE THAMBI : Ombi la mwenye dhambi ni gani?" Ombi la mwenye dhambi ni Ombi ambalo mtu huomba kwa Mungu wakati anapotambua ya kwamba yeye ni mwenye dhambi au ametenda thambi na anahitaji kusamehewa na Mwokozi. Kusema Ombi hili la mwenye dhambi haikamilishi tayari kila kitu. Ombi la mwenye dhambi hufanya kazi tu sawasawa linapokuwa limesimamia kile mtu anacho fahamu, anacho elewa, na kukubali kuhusu dhambi zake na hitaji la Wokovu. Hatua ya kwanza ya Ombi la mwenye dhambi ni kufahamu ya kwamba sisi sote ni wenye dhambi. Warumi 3:10 , “Kama ilivyoandikwa,ya kwamba,Hakuna mwenye haki hata mmoja.” Bibilia inaonyesha wazi ya kwamba sisi sote tumefanya dhambi. Sisi sote ni wenye dhambi na tunahitaji rehema na msamaha toka kwa Mungu (Tito 3:5-7). Kwa ajili ya dhambi zetu,tunastahili adhabu ya milele (Mathayo 25:46). Ombi hili la mwenye dhambi ni kwa kutafuta neema badala ya hukumu. Ni ombi la kuulizia rehema badala ya hasira kuu.rehema ni kuhesabiwa ...

CHANGAMOTO KATIKA LUGHA YA KISWAHILI KWENYE MAMBO YA KOMPYUTA (TEHAMA)

Changamoto zinazoikabili lugha ya Kiswahili katika Teknolojia ya Habari na Mawasiliano Kila jitihada zinazofanywa katika kufikia malengo fulani huwa hakukosi changamoto. Katika jitihada za kufanya Kiswahili kuwa lugha ya kiteknolojia kumetokea changamoto nyingi, moja wapo iliyo kuu kabisa ni kwamba lugha ya Kiswahili haimilikiwi na taifa lolote tajiri kwa hiyo katika harakatika za kuendeleza inakumbana na changamoto nyingi kama vile ukosefu wa fedha na hata utayari wa viongozi wa kisiasa kukiendeleza Kiswahili ni mdogo sana, hata hivyo harakati hizi zinapingwa na mataifa ambayo lugha zao zimeendelea sana kiteknolojia kwa kuhofia kwamba zitafunikwa na matumizi ya Kiswahili. Wapo tayari kutoa misaada ili kuendeleza lugha zao kukididimiza Kiswahili kitu ambacho kinafanya harakati za kukiendeleza Kiswahili kuwa ngumu kwani nchi kinamozungumzwa Kiswahili hazina pesa za kupambana na mataifa makubwa yanayopigia upatu lugha zao. Kutokana na sababu hizo, kasi ya uundaji wa istilahi za kiteknolo...

Serikali ya kishetani

Shetani yuko duniani, na anafanya kazi duniani. Watu wengi wanapokua wanapambana na shetani wanakua wanawaza kwamba yuko mbali sana na wao. Shetani amewakilishwa na majina mbali mbali katika biblia; mfano > Shetani > Ibilisi > Mwovu Shahidi nane kibiblia zinazoonyesha shetani anakaa duniani. 1. Shetani alitupwa duniani Ufunuo 12:12 2. Shimo la kuzimu lipo hapa hapa duniani Ufunuo 9:1-2,11 3. Siku moja alionekana duniani anazunguka zunguka. Ayubu 1:7, ayubu 2:2 Shetani anazunguka zunguka na pia anatembea tembea. Hivyo unaweza kukutana nae anatembea, au anazunguka zunguka. Bwana aliongea na shetani ili sisi tuweze kujifunza kutoka Kwenye maongezi yake. 4. Shetani aligombania mwili kwenye mazishi. Kumbu 34:1-6 Hapa biblia inaonyesha Musa amekufa,na Mungu akamzika. Lakini Yuda 1:9 shetani akashindana na mikaeli kwa ajili ya mwili wa Musa. 5. Shetani aliingia kwenye ibada wakati Kuhani mkuu Yoshua akiendesha ibada Zekaria 3:1-2 6. Shetani aliongea na Daudi. 1 Nyakati 21:1 7. Duni...